Spika za zamani wa bunge la Tanzania Job Ndugai afariki dunia

Ndugai amekuwa Spika wa Bunge tangu November 17, 2015 hadi Januari 06, 2022 alipojiuzulu na kuendelea kuwa Mbunge wa Kongwa ambapo hivi karibuni, alishinda kura za maoni ili aweze kugombea tena nafasi hiyo.

Newstimehub

Newstimehub

6 Agosti, 2025

a61ca148cba6e6d6d7297a02529e4ce49ae3f498bd703ac41c68a9d80d061aeb

Aliyekuwa spika wa zamani wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Job Ndugai amefariki dunia.

Taarifa iliyotolewa na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Tulia Ackson inasema kuwa kifo cha Job Ndugai, kimetokea Agosti 6, 2025.

“Kwa masikitiko makubwa, naomba kutoa taarifa ya kifo cha kiongozi wetu, mwanasiasa mkongwe na Spika mstaafu wa Bunge, Job Ndugai kilichotokea leo jijini Dodoma.