Aliyekuwa spika wa zamani wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Job Ndugai amefariki dunia.
Taarifa iliyotolewa na Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Tulia Ackson inasema kuwa kifo cha Job Ndugai, kimetokea Agosti 6, 2025.
“Kwa masikitiko makubwa, naomba kutoa taarifa ya kifo cha kiongozi wetu, mwanasiasa mkongwe na Spika mstaafu wa Bunge, Job Ndugai kilichotokea leo jijini Dodoma.