Serikali ya Mauritius imesema shambulizi la kombora katika Kisiwa cha Chagos limeongeza wasiwasi kuhusu usalama wa kikanda na kimataifa.
Katika taarifa yake, imesisitiza umuhimu wa kutumia diplomasia badala ya nguvu za kijeshi katika kutatua mgogoro unaoendelea Mashariki ya Kati.
Mgogoro huo, uliosababishwa na mashambulizi kati ya Marekani, Israel na Iran, umeanza kuathiri uchumi wa dunia, hasa sekta ya nishati kutokana na kufungwa kwa njia muhimu za usafirishaji wa mafuta.
CHANZO: Newstimetr














