Mahakama ya Afrika Kusini imewahukumu kifungo cha miaka 20 gerezani raia saba wa China kwa kosa la utekaji nyara na kazi za kulazimishwa, kulingana na taarifa kutoka kwa shirika la habari la serikali.
Walithibitishwa kuwa na hatia mwanzoni mwa mwaka huu kwa utekaji nyara na kazi za kulazimishwa zinazohusisha raia 91 wa Malawi.
Hukumu hii inatokea baada ya kukamatwa kwao miaka sita iliyopita wakati polisi walipotekeleza operesheni ya kukamata watu katika kiwanda kimoja mjini Johannesburg, mji wa kibiashara, ambapo wahamiaji haramu wakiwemo watoto waliopatwa wakifanya kazi chini ya hali mbaya sana, ripoti za SABC zinasema.