Raia wa Afrika kutolipia viza kuingia Burkina Faso

Hata hivyo, urahisi huo unaweza kubadilika baada ya nchi hiyo kujiondoa kutoka Jumuiya ya Kiuchumi ya Nchi za Afrika Magharibi (ECOWAS).

Newstimehub

Newstimehub

12 Septemba, 2025

db307f5928ee8efba35109402bc8269a29e4c446e53b83c8967d13836b3aa7fd

Raia wa Afrika wanaotarajia kuitembelea Burkina Faso, sasa hawatohitaji kulipia gharama za viza.

Hatua hiyo inalenga kukuza muingiliano wa watu na bidhaa ndani ya nchi hiyo, kulingana na Waziri wa Usalama wa Burkina Faso, Mahamadou Sana.

“Kuanzia sasa, raia atokaye nchi yoyote ya Kiafrika, hatolazimika kulipia gharama za viza ili aingie Burkina Faso,” alisema Sana, katika kikao cha baraza la mawaziri kilichoongozwa na Kapteni Ibrahim Traoré siku ya Alhamisi.