Urusi na Madagascar zinalenga kupanua uhusiano katika sekta mbalimbali pamoja na kushirikiana katika majukwaa ya kimataifa.
Rais wa Urusi Vladimir Putin amemkaribisha rais wa Madagascar Michael Randrianirina katika makao ya Kremlin na kuahidi kuimarisha uhusiano wa pande mbili katika sekta nyingi muhimu.
Putin alisisitiza kuwa nchi hizo mbili zina maeneo kadhaa ya ushirikiano yenye fursa kubwa, yakiwemo kilimo, utafiti wa kijiolojia, nishati, tiba, afya na elimu. Alibainisha kuwa vijana kutoka Madagascar tayari wanasoma katika vyuo vikuu vya Urusi na kupata taaluma mbalimbali.
Chanzo: Africanews














