Omar Abdulkadir Artan ameweka historia kwa kuwa mwamuzi wa kwanza wa Kisomali kuchaguliwa kushiriki kwenye mashindano ya Kombe la Dunia la FIFA.
Yeye ni miongoni mwa waamuzi watatu wa kati waliochaguliwa kutoka Afrika na mwakilishi pekee kutoka Afrika Kusini mwa Jangwa la Sahara atakayehudumu katika Kombe la Dunia la FIFA U-20 mwaka 2025.
Mashindano hayo ya kimataifa ya soka yamepangwa kufanyika kuanzia tarehe 27 Septemba hadi 19 Oktoba nchini Chile.