Malkia wa Kenya wapata ushindi dhidi ya Vietnam kwenye voliboli

Timu ya Kenya ya voliboli imeshangaza Poland na Vietnam katika mashindano ya Kombe la Dunia la mchezo huo. Kenya ilionesha umahiri wake na kuwaduwaza zaidi Vietnam.

Newstimehub

Newstimehub

28 Agosti, 2025

1756374722260 o2mo5 e62487ced293616072c6a7b46569f0c8b37fb251a2b8f2211b576e1d12a52730

Licha ya kuwa vinara wa mashindano ya barani Afrika wakiwa na mataji kumi, Malkia Strikers wamekuwa hawafanyi vizuri katika jukwaa la Dunia.

Siku ya Jumatano waliishinda Vietnam kwa seti 3-0 (25-23, 25-22, 25-18) kuwafanya wapate ushindi wao wa tatu katika mechi kumi walizocheza mashindano ya Dunia.