Mahakama ya ICC kuanza kusikiliza kesi ya Joseph Kony

Kony anakabiliwa na mashitaka 39 ya uhalifu wa kivita na dhidi ya ubinadamu, yakiwemo mauaji, ubakaji, utumwa wa kingono, na utekaji wa watoto.

Newstimehub

Newstimehub

8 Septemba, 2025

1a8acee114c59c12b7c68a3483b8f2ee3e5cef1bdc00dd176f7bc7268268daa1

Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu (ICC) siku ya Jumanne, itasikiliza kesi ya kihistoria dhidi ya Joseph Kony, kiongozi wa kundi la waasi la Lord’s Resistance Army (LRA), ambaye amekuwa mafichoni kwa zaidi ya miaka 30.

Kony anakabiliwa na mashitaka 39 ya uhalifu wa kivita na dhidi ya ubinadamu, yakiwemo mauaji, ubakaji, utumwa wa kingono, na utekaji wa watoto.