Mahakama Kuu ya Eswatini imetupilia mbali kesi iliyowasilishwa na wanaharakati wa haki za binadamu waliopinga mpango wa kupokea wahamiaji waliotumwa kutoka Marekani.
Watetezi hao wamekata rufaa dhidi ya uamuzi huo huku wakisema mpango huo unaibua maswali ya haki za binadamu.
Kwa sasa, baadhi ya wahamiaji waliowasili nchini humo bado wanazuiliwa gerezani licha ya kumaliza vifungo walivyotumikia nchini Marekani.
CHANZO: Newstimetr














