Zaidi ya maambukizi 100,000 ya kipindupindu yameripotiwa katika taifa la Sudan kwenye kipindi cha mwaka mmoja uliopita, Ofisi ya Umoja wa Mataifa inayoshughulikia masuala ya misaada kwa watu (OCHA) ilisema Jumatatu.
“Sudan inakabiliwa na janga baya la njaa kote duniani, huku kipindupindu kikiongezeka. Njaa kali imethibitishwa katika baadhi ya sehemu za nchi,” OCHA imesema katika taarifa kwenye mtandao wake wa X wa Marekani.
“Hatuwezi kusimama tu hapa, watu wa Sudan wanahitaji msaada,” iliongeza, akiutaja mlipuko wa kipindupindu “kuwa mkubwa” katika miaka ya hivi karibuni.








