Maafisa waliofariki katika ajali ya helikopta Ghana wazikwa

Waziri wa Mazingira, Sayansi na Teknolojia Ibrahim Murtala Muhammed na Naibu Mratibu wa Usalama Limuna Muniru Mohammed walizikwa siku ya Jumapili.

Newstimehub

Newstimehub

11 Agosti, 2025

dafb1b87ba0dc5efff1b3628fce5fee10f7c9b6778ace698f6de63a12e3acf41

Mamlaka nchini Ghana zimefanikiwa “kutambua vyema” miili minane ya maafisa wa serikali waliofariki katika ajali ya helikopta ya jeshi siku ya Jumatano na kufanya mazishi ya watwili wao.

Mazishi ya Waziri wa Mazingira, Sayansi na Teknolojia Ibrahim Murtala Muhammed na Naibiu Mratibu wa Usalama Limuna Muniru Mohammed, yalifanyika siku ya Jumapili, Agosti 10, Shirika la Habari la Ghana liliripoti.

Mazishi hayo ya kitaifa yaliyoongozwa na Rais John Mahama yalifanyika Ikulu mjini Accra na viongozi wengine walihudhuria ikiwemo Rais wa Sierra Leone Julius Maada Bio na Mwenyekiti wa ECOWAS kwa viongozi wa Nchi na Serikali.

“Kwa hiyo tubadilishe huzuni hiyo na kuwa kichocheo cha kuchukua hatua. Tuwaenzi, sito kwa kutoa machozi, lakini kwa kukumbuka waliyoyafanya wakiwa hai na kile amacho wamekufia … Walitumikia Ghana kwa moyo wao wote, na ni jukumu letu kuendeleza huduma hiyo,” Mahama alisema wakati wa hafla hiyo.