Kipa wa Manchester City Ederson, amekamilisha uhamisho wake kuelekea klabu ya Fenerbahce ya nchini Uturuki.
Hayo yanajiri wakati mtaliano Gianluigi Donnarumma akijiandaa kwenda kuchukua nafasi ya Ederson ndani ya Manchester City kwa dau la Dola Milioni 41, baada ya kuambiwa kuwa ‘hahitajiki tena’ na klabu ya Paris Saint-Germain (PSG) ya Ufaransa, licha ya kuisaidia kutwaa Ligi ya Mabingwa Ulaya msimu uliopita.
Kwa upande mwingine, City ilimnunua golikipa wa Burnley, James Trafford mwishoni mwa msimu, licha ya muingereza huyo kushindwa kuonesha makali yake.
