Hussein Mwinyi atangazwa mshindi wa Urais Zanzibar

Mpinzani wake wa chama cha ACT Wazalendo Othman Masoud Othman ameshika nafasi ya pili.

Newstimehub

Newstimehub

30 Oktoba, 2025

958c731f6ce49b1ab646ef0d6eb1e5150ac144605a4528b3830a17c7a12e8856

Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC) imemtangaza mgombea wa Chama Cha Mapinduzi (CCM), Hussein Ali Mwinyi, kuwa mshindi wa uchaguzi wa urais wa Zanzibar. Mwinyi amejipatia jumla ya kura 448,892, sawa na asilimia 74.8 ya kura.

Mgombea wa chama cha ACT-Wazalendo, Othman Masoud Othman, ameshika nafasi ya pili kwa kupata kura 139,399, ambazo ni sawa na asilimia 23.2.

Zanzibar ni sehemu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, inayojumuisha visiwa vikuu vya Unguja na Pemba, vilivyoko katika Bahari ya Hindi, mashariki mwa pwani ya Tanzania bara.