Rais wa Afrika Kusini, Cyril Ramaphosa, ameongoza mazishi ya mabaki ya raia 63 waliorejeshwa kutoka Ulaya, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kitaifa za kurejesha haki kwa jamii za asili.
Mabaki hayo, yaliyotoka kwa jamii za Khoi na San, yalichukuliwa kinyume cha maadili wakati wa ukoloni na kuhifadhiwa katika makumbusho na vyuo vikuu.
Hatua hiyo imeelezwa kuwa ni sehemu ya mpango mpana wa kurejesha urithi wa Afrika na kuhakikisha wahanga wa ukoloni wanaheshimiwa ipasavyo.
CHANZO: Newstimetr














