CCM yaadhimisha miaka 49 tangu kuanzishwa

Chama cha Mapinduzi (CCM) nchini Tanzania chaadhimisha miaka 49 tangu kuanzishwa kwake.

Newstimehub

Newstimehub

5 Februari, 2026

f05530a7ec0a2c903038819ac04286c8e9417f7ce894da21e3d64a89daa68082

Makamu wa Rais wa Tanzania, Dkt. Emmanuel Nchimbi, amehudhuria maadhimisho hayo yaliyofanyika leo Februari 5, 2026 katika Wilaya ya Chemba, mkoani Dodoma.

Akizungumza katika maadhimisho hayo, Dkt. Nchimbi ametoa wito kwa wanachama wa CCM kutekeleza wajibu wao wa msingi na wa kudumu kwa kuhakikisha chama kinaendelea kuwa cha Watanzania wote na kuwa ndio kimbilio lao.

Dkt. Nchimbi amesema kuwa kila mwanachama na kiongozi wa CCM anatakiwa kutafakari matendo yake na namna yanavyochangia maendeleo, kuimarisha umoja na mshikamano wa chama pamoja na Taifa kwa ujumla.

Aidha, Dkt. Nchimbi amesema kuwa wakati chama kikielekea katika uchaguzi wa ndani kuanzia ngazi ya shina hadi Taifa mwaka 2027, ni muhimu kwa wanachama kuanza kujiandaa mapema kwa kuzingatia misingi muhimu ikiwemo kulinda maadili ya chama, kudumisha umoja na mshikamano, kuendeleza amani na utulivu, pamoja na kutambua kuwa uongozi ni dhamana ya kuwatumikia wananchi.