Baraza la Masuala ya Kisiasa na Usalama la Umoja wa Afrika lilitoa wito siku ya Jumanne “kufutwa mara moja” kwa Israel kuitambua Somaliland.
Waziri wa Mambo ya Nje wa Israel Gideon Sara alitembelea Somaliland siku ya Jumanne katika safari ambayo ililaaniwa na Somalia, siku 10 baada ya Israel kulitambua rasmi eneo hilo lililojitangaza kuwa taifa huru.
“Baraza la (AU) linalaani vikali, kwa maneno makali zaidi, utambuzi wa upande mmoja wa kile kinachojulikana kama ‘Jamhuri ya Somaliland’ na Israel,” ilisema kwenye chapisho kwenye X baada ya mkutano wa mawaziri.









