Raia wa Rwanda afunguliwa mashtaka Marekani kwa kuhusika na mauaji ya kimbari

Kama inavyodaiwa katika hati ya mashtaka, Faustin Nsabumukunzi aliyeishi Mareknai tangu 2003, alitumia nafasi yake ya uongozi akiwa Rwanda kusimamia ghasia na mauaji ya Watutsi.
25 Aprili, 2025
Dunia yaadhimisha siku ya malaria, nchi 9 Afrika bila malaria

Barani Afrika WHO inasema tangu mwaka wa 2000, zaidi ya wagonjwa wa malaria bilioni 1.7 na vifo milioni 12 vimepukwa katika kanda ya Afrika kutokana na juhudi za kimataifa za afya.
25 Aprili, 2025
Marekani kuwa mwenyeji wa makubaliano kati ya Rwanda na DRC

Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani Marco Rubio atatia saini ‘tamko la kanuni’, siku chache baada ya kutangazwa kusitishwa kwa mapigano kati ya DRC na waasi wa M23 wakati wa mazungumzo ya hivi karibuni yaliyofanywa na Qatar huko Doha.
25 Aprili, 2025
Kenya yaamua tena hisabati kuwa somo la lazima

Haya yanajiri baada ya Wizara ya Elimu kutangaza kuwa masomo ya hesabu hayatakuwa ya lazima tena kwa wanafunzi wa sekondari chini ya Mtaala unaozingatia Umahiri (CBC), mabadiliko makubwa kutoka kwa mfumo ulioondolewa wa elimu.
25 Aprili, 2025

Msumbiji yatangaza kumalizika kwa uasi katika mkoa wenye utajiri wa gesi wa Cabo Delgado

Rais wa Afrika Kusini Ramaphosa kukutana na Trump ‘karibuni’ kusuluhisha matatizo yao

Magaidi wa al-shabaab wavamia kambi ya jeshi Somalia, watu kadhaa wauawa

Jeshi la Sudan lasema limewaua wapiganaji 60 wa RSF Darfur Kaskazini

Rais wa Ukraine kukatisha ziara yake ya Afrika Kusini
24 Aprili, 2025
Rwanda yazindua mikakati mipya ya kuthibiti malaria
Mbinu mpya inahusisha kupima familia yote baada ya mtu mmoja kugundulika kuwa na ugonjwa wa malaria ili kutambua na kutibu wengine ambao wanaweza kuambukizwa lakini bado hawana dalili.

24 Aprili, 2025
Mahakama ya Senegal yazuia ombi la serikali la kufuta sheria ya msamaha kwa ‘wahalifu’
Baraza la Katiba la Senegal lilitangaza sheria mpya ya msamaha kuwa kinyume na katiba, na hivyo kuzua mvutano mpya wa kisiasa kati ya wapinzani.

24 Aprili, 2025
Serikali ya DRC, M23 wakubali kufanya mazungumzo
Taarifa iliyotolewa katika mazungumzo imethibitisha kwamba pande zote mbili zimekubaliana kusitisha mapigano mara moja.

23 Aprili, 2025
Wabelgiji, Mvietnam,Mkenya waliopatikana na siafu, kuhukumiwa mwezi ujao
Washukiwa hao wanne wamekiri makosa yao wiki iliyopita baada ya mamlaka kuwakamata wakiwa na siafu 5,000.

23 Aprili, 2025
Djibouti yawapa wahamiaji haramu wiki moja kuondoka au wawaondowe kwa lazima
Raia wengi wa kigeni wanapitia nchi hiyo kwa lengo la kuanza safari ya hatari kupitia Bahari ya Shamu kwa kutumia maboti yaliyojaa kupitiliza.

23 Aprili, 2025
Wafugaji wenye silaha wawaua watu 11 katika mashambulizi mengine Nigeria
Kumekuwepo na ongezeko la mapigano katika eneo hilo katika kipindi cha miezi kadhaa iliyopita kati ya wakulima na wafugaji

23 Aprili, 2025
Rais Ruto asaini mikataba 7 na Uchina ya uwekezaji wa zaidi ya dola milioni 823
Sekta ya kibinafsi ya Uchina imekuwa muhimu katika kukuza ukuaji wa uchumi wa Kenya kwa miaka mingi kupitia uwekezaji wao katika sekta mbalimbali za uchumi wetu- Ruto

23 Aprili, 2025
Kenya kuunda kitengo maalum kukabiliana na usafirishaji haramu wa binadamu
Kamati ya Kudumu ya Seneti ya Kenya kuhusu Kazi na Ustawi wa Jamii inaripoti kuwa takriban wafanyakazi 80,000 wa Kenya wako Saudi Arabia na 60,000 katika Umoja wa Falme za Kiarabu (UAE), wengi wao wakiwa wafanyakazi wa nyumbani

23 Aprili, 2025
Mataifa matatu ya Sahel kujiondoa kutoka Ecowas ‘inasikitisha’ – rais wa Ghana
Rais John Mahama anatoa wito wa “uimara zaidi na uelewano kwa ajili ya changamoto ngumu zinazowakabili ndugu zetu katika mataifa ya Sahelian.”

22 Aprili, 2025
Watu 3 wamefariki, na mamia wengine kuondoka katika makazi yao kutokana na mafuriko Nairobi, Kenya
Mwanamke mmoja, na watoto wake 2 walifariki baada ya kuangukiwa na ukuta wakati wa mvua kubwa



