Kamanda wa jeshi la Sudan atoa wito wa kuhamasisha umma dhidi ya RSF

Kamanda mwandamizi wa jeshi la Sudan ametoa wito kwa raia kuitikia ombi la kiongozi wa jeshi Abdel Fattah al-Burhan wa kutaka waungane nchini nzima dhidi ya wapiganaji wa RSF.
20 Novemba, 2025
Trump kuanza jitihada za kusitisha vita Sudan

Rais wa Marekani Donald Trump alisema Jumatano kuwa ataanza “kufanyia kazi” vita vya Sudan, baada ya Mwanamfalme wa Saudi Arabia, Mohammed bin Salman, aliyekuwa ziarani Marekani, kumwomba kusaidia kumaliza mgogoro huo.
19 Novemba, 2025
Maafisa 2 wa Kenya wamefariki baada ya gari lao kukanyaga bomu lililotegwa na kundi la al-Shabab

Maafisa wawili wa Kikosi cha Ulinzi wa Mipakani nchini Kenya wamefariki siku ya Jumatano baada ya gari lao kukanyaga bomu lililotegwa ardhini (IED) na wanamgambo wa al-Shabab wanaotoka Somalia, kwa mujibu wa polisi wa Kenya.
19 Novemba, 2025
Arsenal kusitisha ushirikiano wake na Visit Rwanda

Baada ya miaka nane ya nembo ya Visit Rwanda kupamba bega la jezi za Arsenal, klabu hiyo ilitangaza kuwa itasitisha mkataba wa udhamini na Visit Rwanda ifikapo mwezi Juni 2026.
19 Novemba, 2025

Rais wa Nigeria athibitisha kuuawa kwa jenerali wa jeshi

Wataalamu wa Afrika watoa wito wa kukaguliwa tathmini ya viwango vya mikopo kwa bara

Eswatini yapokea dola milioni 5.1 kupokea wahamiaji waliofurushwa Marekani, waziri anasema

Gabon yatia saini makubaliano ya kihistoria ya ufadhili wa hali ya hewa kwa misitu ya mvua ya Congo

Jeshi la Somalia limewauwa magaidi 11 wa Al Shabab na kuzuia shambulio la kujitoa muhanga
18 Novemba, 2025
Tanzania huenda ikakabiliwa na changamoto kupata mikopo kutoka nje, amesema Rais Samia
Uwezo wa Tanzania kupata mikopo kutoka taasisi za kimataifa huenda ukakumbana na changamoto baada ya sifa yake kuharibika kimataifa, amesema Rais Samia Suluhu Hassan siku ya Jumanne wakati wa kuwaapisha mawaziri.

18 Novemba, 2025
Sura mpya Baraza la Mawaziri Tanzania
Taifa hilo limeshuhua kuapishwa kwa baraza jipya la mawaziri, Novemba 18 huku kukiwa na maingizo mapya katika baraza hilo lenye jumla ya wizara 27.

18 Novemba, 2025
Cape Verde, Mauritius na Ushelisheli wafanikiwa kuangamiza surua na rubela
WHO imetangaza kuangamizwa kwa magonjwa ya Surua na Rubela nchini Mauritius, Ushelisheli na Cape Verde, ikiwa ni mara ya kwanza kwa mafanikio hayo kusini mwa jangwa la Sahara.

18 Novemba, 2025
Zaidi ya watu 100,000 wamekimbia makazi yao kutoka Al Fasher ya Sudan tangu kutwaliwa na RSF
Zaidi ya raia 100,000 wamefurushwa kutoka kwa Al Fasher magharibi mwa Sudan tangu kuchukuliwa kwa mji huo na Wanajeshi wa Msaada wa Haraka (RSF) mwezi uliopita, IOM imesema.

17 Novemba, 2025
Rais wa Tanzania amteua binti na mkwe wake katika Baraza la Mawaziri
Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, amemteua binti yake, Wanu Hafidh Ameir, kuwa Naibu Waziri wa Elimu. Hafidh Ameir, mwenye umri wa miaka 43, ni Mbunge wa Jimbo la Makunduchi.

17 Novemba, 2025
Rais Samia amteua waziri mpya wa fedha, awaacha mawaziri wa mambo ya nje na madini madarakani
Rais wa Tanzania, Samia Suluhu Hassan, Jumatatu alimteua balozi wa nchi hiyo nchini China, Khamis Mussa Omar, kuwa waziri wa fedha katika baraza lake jipya la mawaziri kufuatia uchaguzi uliokumbwa na utata mwezi uliopita.

17 Novemba, 2025
Tovuti za taasisi za serikali ya Kenya zashambuliwa
Mashambulizi hayi yalilenga baadhi ya mashirika ya serikali yanayotoa huduma muhimu.

17 Novemba, 2025
Mgodi waporomoka DRC na kuua watu wasiopungua 32
Daraja lililoporomoka katika mgodi wa cobalt kusini mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (DRC) na kuua wachimba migodi 32, afisa wa serikali ya mkoa alisema Jumapili.

16 Novemba, 2025
Wahamiaji 4 wafariki baada ya boti mbili zilizokuwa zimebeba makumi ya watu kuzama pwani ya Libya
Wahamiaji wanne walifariki baada ya boti mbili zilizokuwa zimebeba karibu watu 100 kupinduka katika pwani ya Al-Khums kaskazini magharibi mwa Libya, Shirika la Hilali Nyekundu la Libya lilisema Jumamosi jioni.

16 Novemba, 2025
Kikundi cha matabibu kinaripoti visa ya ubakaji wa wasichana wa Al Fasher baada ya RSF kuteka
Mtandao wa Madaktari wa Sudan unasema ubakaji “ni sawa na uhalifu wa kivita na uhalifu dhidi ya ubinadamu.”



