Wabunge wa Afrika Mashariki wapongeza ushindi wa Rais Samia

Pongezi hizo zinakuja wiki moja kabla ya wakuu wa nchi za Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) hawajakutana jijini Nairobi.
28 Novemba, 2025
Rais wa Guinea-Bissau awasili Senegal baada ya jeshi kufanya mapinduzi

Senegal imethibitisha kuwa Embalo aliwasili mjini Dakar “akiwa salama” baada ya mapinduzi kuzuia kutangazwa kwa matokeo ya uchaguzi nchini Guinea-Bissau.
28 Novemba, 2025
Umoja wa Afrika wataka Rais wa Guinea-Bissau aachiwe mara moja

Umoja wa Afrika umetoa wito wa kuachiliwa “mara moja na bila masharti” kwa Rais wa Guinea-Bissau, Umaro Sissoco Embaló, baada ya jeshi kuchukua mamlaka ya nchi hiyo kwa nguvu.
27 Novemba, 2025
Rais Kagame aishutumu DRC kwa kuchelewesha makubaliano ya amani ya Washington

Rais wa Rwanda Paul Kagame ameishutumu serikali ya Congo kwa kuchelewesha kutia saini makubaliano ya amani yenye lengo la kumaliza mzozo katika eneo lenye utajiri wa madini mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.
27 Novemba, 2025

Kiongozi wa mapinduzi Guinea-Bissau, atangazwa kuwa ‘Rais wa mpito’

Mwanamke Mjerumani afungwa jela DRC kwa wizi wa benki

Trump aipiga marufuku Afrika Kusini kuhudhuria mkutano wa G20 Miami 2026

Rais wa Nigeria atangaza hali ya dharura kufuatia utekaji uliokithiri

Kiongozi wa jeshi la Sudan atoa wito kwa Trump asaidie kusitisha vita nchini humo
26 Novemba, 2025
Jeshi lasitisha mchakato wa uchaguzi nchini Guinea-Bissau, latangaza kuchukua udhibiti
Maafisa wa jeshi wanaojiita “Uongozi wa Juu wa Kijeshi kwa Marejesho ya Utulivu” wamesitisha uchaguzi, vipindi vya vyombo vya habari, huku wakilitaka taifa “liwe na utulivu,” kwa mujibu wa chombo cha habari cha serikali.

26 Novemba, 2025
Hatimaye mlipuko wa volkano ya Hayli Gubbi ya Ethiopia wapungua
Huu ni mlipuko wa kwanza uliorekodiwa wa Hayli Gubbi katika miaka 10,000 iliyopita,” aliambia, na Inawezekana itaendelea kwa muda mfupi na kisha itasimama hadi mzunguko unaofuata.

26 Novemba, 2025
Jeshi la Sudan linasema kuwa limezuia mashambulizi ya RSF kwenye mji muhimu
Jeshi la Sudan lilisema siku ya Jumanne kuwa limezuia mashambulizi ya Vikosi vya Msaada wa Haraka (RSF) kwenye mji wa kimkakati wa Kordofan kusini, siku moja baada ya RSF kutangaza kusitisha mapigano kwa muda wa miezi mitatu kwa upande mmoja.

26 Novemba, 2025
Kampuni ya mafuta ya serikali ya Uganda yagundua hifadhi mpya ‘muhimu’
Kampuni ya Kitaifa ya Mafuta ya Uganda (UNOC) inayomilikiwa na serikali imetambua visima tisa vya mafuta katika mtaa wa Kasuruban na “akiba mpya ya mafuta ghafi”, ilisema Jumanne.

25 Novemba, 2025
Wasichana wa shule waliotekwa Nigeria wameachiwa huru
Wasichana 24 waliotekwa katika shule kaskazini-magharibi mwa Nigeria wiki iliyopita wameachiwa huru, msemaji wa gavana wa jimbo la Kebbi alisema siku ya Jumanne.

25 Novemba, 2025
Watu 10 zaidi watekwa nyara Nigeria
Watekaji nyara wamewateka wanawake na watoto 10 katika tukio jipya la utekaji nyara nchini Nigeria, polisi wamesema siku ya Jumanne.

25 Novemba, 2025
Wafuasi 300 wa upinzani wamekamatwa wakati wa kampeni nchini Uganda
Vyombo vya usalama nchini Uganda vimewakamata wafuasi na maafisa zaidi ya 300 kutoka chama cha mgombea wa urais wa upinzani Bobi Wine tangu kampeni za uchaguzi wa Januari kuanza mwezi uliopita, alisema msemaji wa chama hicho Jumanne.

25 Novemba, 2025
Ndege iliyobeba msaada wa chakula yaanguka Sudan Kusini, watatu wafariki
Ndege iliyokuwa ikisafirisha msaada wa chakula kwa shirika la kimataifa la Samaritan Purse ilianguka katika Jimbo la Unity nchini Sudan Kusini siku ya Jumanne, wafanyakazi wake wote watatu wamefariki, afisa wa shirika hilo amesema.

25 Novemba, 2025
Mwanajeshi wa zamani wa Uingereza anayesakwa nchini Kenya kwa mauaji anyimwa dhamana
Mwili wa Wanjiru ulipatikana kwenye tanki la maji taka katika Hoteli ya Lion’s Court katika mji wa Nanyuki nchini Kenya mnamo Juni 2012. Wanjir alionekana mara ya mwisho akiwa na kundi la wanajeshi wa Uingereza usiku wa Machi 31 na Aprili 1, 2012.

25 Novemba, 2025
Marekani yaondoa ushuru wa 15% kwa kakao ya Ghana, mauzo ya nje
Ghana imepata uthibitisho rasmi kutoka Marekani kwamba Washington imeondoa kikamilifu ushuru wa asilimia 15 uliowekwa kwa mauzo ya nje ya kakao na mazao mengine katika taifa hilo la Afrika Magharibi.



