Mchezaji wa PSG na timu ya taifa ya Morocco anakabiliwa na kesi ya ubakaji inayotokana na tukio la Februari 2023, huku akiendelea kukanusha vikali tuhuma hizo.
Mchezaji wa kimataifa wa Morocco na klabu ya PSG, Achraf Hakimi, amefikishwa katika mahakama ya uhalifu ya Hauts-de-Seine nchini Ufaransa kujibu tuhuma za ubakaji zinazodaiwa kutokea Februari 2023.
Kesi hiyo imefika hatua ya kusikilizwa mahakamani baada ya karibu miaka mitatu ya uchunguzi wa kisheria. Hakimi amekanusha vikali tuhuma zote zinazomkabili.
Mamlaka za Ufaransa zinasema uchunguzi ulipelekea kuamuliwa kuwa kesi hiyo ifikishwe mahakamani, ambapo uamuzi wa mwisho utatolewa na jopo la majaji.
Chanzo: AA














