Viongozi wa afya barani Afrika wameeleza wasiwasi kuhusu mwelekeo mpya wa misaada ya Marekani kupitia mikataba ya moja kwa moja na nchi binafsi, wakihofia kuwa data za kiafya za Waafrika zinaweza kutumiwa vibaya.
Kwa mujibu wa viongozi hao, baadhi ya mataifa ya Afrika yana wasiwasi kwamba taarifa za kiafya zinaweza kukusanywa na kutumika kutengeneza tiba au bidhaa za kitabibu ambazo baadaye hazitashirikishwa kwa haki na nchi zilizotoa data hiyo.
Rais wa World Health Summit Axel Pries amesema data za afya hazipaswi kuwa bidhaa ya biashara inayotumiwa katika makubaliano ya kisiasa au kifedha.
Tahadhari hiyo imeongeza mjadala kuhusu umuhimu wa Afrika kuwa na udhibiti kamili wa taarifa zake za kiafya na mifumo yake ya afya.
CHANZO: Newstimetr














