Wamisri wasiopungua 14 wafariki baada ya boti la wahamiaji kuzama Crete: Cairo

Wamisri wasiopungua 14 wamefariki baada ya boti la wahamiaji kuzama karibu na bandari katika kisiwa cha Crete cha Ugiriki, Wizara ya Mambo ya Nje ilisema siku ya Jumanne.

Newstimehub

Newstimehub

16 Desemba, 2025

77a8d444d5e83b5e2446b848d80fa21738f24baf06d7090d67635e960a8f0d03

Wamisri wasiopungua 14 wamefariki baada ya boti la wahamiaji kuzama karibu na bandari katika kisiwa cha Crete cha Ugiriki, Wizara ya Mambo ya Nje ilisema siku ya Jumanne.

Katika taarifa, wizara ilisema inafuatilia kuzama kwa boti la wahamiaji lililoondoka kutoka nchi jirani ya Misri likielekea Ugiriki Disemba 7, 2025.

Boti hilo lilikuwa limebeba wahamiaji 34 kutoka mataifa mbalimbali, ikiwemo 14 kutoka Misri ambao walifariki, wizara iliongeza.

Wizara inasema iliwasiliana mara moja na mamlaka za Ugiriki kwa ajili ya kutoa msaada wowote unaohitajika kwa wale waliookolewa kutoka kwenye boti hiyo, na kusafirisha miili ya raia wa Misri.

Tukio ‘baya’

Akieleza tukio hilo kama “baya,” wizara ilitoa wito kwa raia wa Misri “kutohadaiwa na mitandao ya uhamiaji haramu,” ili kulinda maisha yao na kuepuka matukio kama hayo ya uchungu kutokea tena.

Wahamiaji haramu wamekuwa wakitumia Libya na mataifa jirani kufikia kisiwa cha Crete, njia ya kufika nchi za Muungano wa Ulaya.

Mapema mwezi Julai, serikali ya Ugiriki iliamua kufuta maombi ya wanaoomba hifadhi ya kisiasa, hasa wale wanaowasili Crete kutoka Libya.

Misri inasema imezuia kuondoka kwa maboti ya wahamiaji yanayoelekea Ulaya tangu 2016, huku wahamiaji haramu kutoka Misri wakitumia njia ya Libya.