Rais Salva Kiir awafukuza kazi mawaziri wake watatu

Taifa hilo, ambalo lilijitenga kutoka Sudan mwaka 2011, limekumbana na hali ya machafuko kufuatia kuhasimiana kati ya Kiir na Naibu wake, Riek Machar uliopelekea kuanzishwa kwa makubaliano ya kugawana madaraka, mwaka 2018.

Newstimehub

Newstimehub

2 Septemba, 2025

ae39cdede3f92c97c8aff0208b3f11e211d95f10b31883cd23fda27502fd434c

Rais wa Sudan Kusini Salva Kiir amewaachisha kazi mawaziri wake watatu, akiwemo na gavana wa jimbo la magharibi la Bahr el Ghazal, katika mabadiliko aliyoyafanya kwenye baraza lake la mawaziri siku ya Jumatatu.

Kupitia tamko take lililorushwa na Shirika la Utangazaji la Sudan Kusini (SSBC), Salva Kiir amemfuta kazi Waziri wake wa Sheria Wek Mamer Kuol na kumteua Joseph Geng Akec kama mbadala wake.

Katika hatua hiyo hiyo, Kiir amemteua Mary Nawai kama Waziri wa Vijana na Michezo, akichukua nafasi ya Akec.