Takriban watu 70 waliuawa wakati mashua iliyokuwa imebeba wahamiaji ilipopinduka katika pwani ya Afrika Magharibi, wizara ya mambo ya nje ya Gambia ilisema Ijumaa jioni, katika moja ya ajali mbaya zaidi katika miaka ya hivi karibuni kwenye njia maarufu ya wahamiaji kuelekea Ulaya.
Watu wengine 30 wanahofiwa kufariki baada ya meli hiyo, inayoaminika kuondoka Gambia na kuwabeba raia wengi wa Gambia na Senegal, kuzama katika pwani ya Mauritania mapema Jumatano, wizara ilisema katika taarifa yake.
Ilikuwa imebeba takriban abiria 150, 16 kati yao walikuwa wameokolewa. Mamlaka ya Mauritania ilipata miili 70 siku ya Jumatano na Alhamisi, na takwimu kutokana na mashahidi zinaonyesha zaidi ya 100 wanaweza kuwa wamekufa, taarifa hiyo ilisema.














