Jiwe la zumaridi lenye uzito wa karati 11,685 (kilo 2.3) limegunduliwa nchini Zambia, kampuni moja ya uchimbaji imetangaza.
“Kwa uzito wa karati 11,685, Imboo (nyati) ni jiwe la thamani la hivi karibuni na kubwa zaidi lililogunduliwa katika Mgodi wa Kagem (Kagem), unaoaminika kuwa mgodi mmoja mkubwa zaidi wa kuzalisha zumaridi duniani,” Gemfields ilisema katika taarifa yake.
Imboo iligunduliwa katika shimo la Chama la Kagem mnamo Agosti 3, 2025 na mtaalamu wa jiolojia Dharanidhar Seth, ambaye ana uzoefu wa zaidi ya muongo mmoja, pamoja na Justin Banda, mchongaji stadi ambaye amekuwa muhimu katika kugundua mawe mengi ya thamani.