Ujumbe wa Umoja wa Mataifa katika Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo (MONUSCO) umeshtumu “vikali” mashambulizi yaliyofanywa na kundi la Allied Democratic Forces (ADF) ambayo yaliwaua raia wasiopungua 52 mashariki mwa nchi.
ADF ililenga maeneo ya Beni na Lubero katika mkoa wa mashariki wa Kivu Kaskazini kuanzia Agosti 9 – 16 ikiwemo mauaji ya wanawake wanane na watoto wawili, taarifa ya MONUSCO ilisema siku ya Jumatatu.
Bintou Keita, mwakilishi maalum wa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Congo na kiongozi wa MONUSCO, anasema mashambulizi, yanakuja baada ya mashambulizi ya ADF katika kanisa moja mwishoni mwa mwezi Julai, ambayo yalikuwa “ni ukiukwaji mkubwa wa sheria za binaadamu za kimataifa,.”