Serikali ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo na waasi wa M23 wameshindwa kufikia makubaliano ya amani ya Doha katika siku ya mwisho ya kufanya hivyo, kuongeza wasiwasi kati ya makundi hayo mawili kuwa mazungumzo yanaweza kutatizwa na kurejesha nyumba hatua zilizopigwa za kumaliza mapigano.
Mapigano mashariki mwa DRC yameongezeka mwaka huu, huku kundi la M23 likianzisha mapigano na kuchukuwa udhibiti wa miji mikubwa miwili.
Chini ya juhudi za upatanishi ziloongozwa na Qatar, DRC na waasi hao walitia saini azimio la makubaliano Julai 19 ambapo waliapa kuanza mashauriano kabla ya Agosti 8 na kwa lengo la kufikia Agosti 18.
Waasi wa M23 walisema katika taarifa Jumapili kuwa utekelezaji wa azimio, ambapo unajumuisha kuwaachia huru wafungwa, kungesaidia kuendelea na hatua nyingine ya mazungumzo.
Makubaliano