Wagombea zaidi wa Urais Tanzania wapokea fomu zao za uteuzi kutoka kwa Tume huru ya Uchaguzi

Miongoni mwa wagombea waliokabidhiwa fomu zao za kugombea urais na makamu wa rais, ni George Gabriel Bussungu kupitia tiketi ya Chama cha Tanzania Democratic Alliance (TADEA).

Newstimehub

Newstimehub

11 Agosti, 2025

a118771bfdc49a3026dc1bf0f3513e35d950e8abb4a804c7a7646522330bc64c

Vyama mbalimbali vya kisiasa nchini Tanzania vinaendelea kuchukua fomu za wagombea wa kiti cha urais pamoja na makamu wake.

Miongoni mwa wagombea urais waliokabidhiwa fomu na Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi Tanzania za kugombea kiti cha urais na makamu wa rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Agosti 11, 2025, ni George Gabriel Bussungu kupitia tiketi ya Chama cha Tanzania Democratic Alliance (TADEA).

Bussugu aliambatana na mgombea wake mwenza, Ali Makame Issa.

Kwa mujibu wa kalenda ya INEC, dirisha la kuchukua fomu hizo kwa nafasi ya uraia litakamilika Agosti 27.